Tuesday, December 29, 2009

Simba kuteta mwishoni mwa wiki

#Ni kujadili mabao mawili ya Yanga
Na Badru Kimwaga
VIONGOZI wa klabu ya Simba wanatarajia kuwekana 'kitimoto' na kujadili kipigo cha Yanga katika kikao chao cha Kamati ya Utendaji kitakachofanyika mwishoni mwa wiki.
Viongozi na wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji wameshajulishwa kikao hicho muhimu, ambacho pia kitatoa nafasi ya kujadili mambo mengine muhimu ya maendeleo ya klabu.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya klabu ya Simba, ni kwamba kikao hicho ambacho ni muendelezo ya kikao kilichofanyika awali Novemba 30 kitafanyika kwenye hoteli ya Regency.
Kubwa litakaloongelewa kwenye kikao hicho ni kipigo toka Yanga, uchaguzi mkuu na hoja ya mapato na matumizi ambayo imekuwa ikilalamikiwa kwa muda mrefu sasa.
Kamati hiyo inaundwa na Ayoub Semvua, Omar Gumbo, Mohammed Mjenga na Hassan Othman 'Hassanoo', iliyopewa kazi ya kukutana na TFF kwa lengo la kufanyia marekebisho ya katiba yao kabla ya kuitishwa kwa uchaguzi mkuu.
Mmoja wa wajumbe wa kamati ya utendaji, Said 'Seydou' Rubeya, alithibitisha kupata barua ya mualiko wa kikao hicho na kusisitiza anaenda kwenye kikao hicho kutaka majibu ya ombi lake juu ya mapato na matumizi ya klabu yao.

No comments:

Post a Comment