Wednesday, December 23, 2009

Simba yatamba kuitafuna Yanga

BAADA ya kuanza vizuri kwenye michuano ya Tusker, Simbari, imesema imejiwekea malengo ya kushinda mchezo wa kesho dhidi ya Yanga wa nusu fainali ya Kombe la Tusker ili kudumisha rekodi yake iliyoianza katika Ligi Kuu Bara.
Simba inaongoza ligi hiyo ikiwa na uhakika na imesema dhamira ya kushinda mchezo wa kesho inatokana na ubora wa wachezaji wake akiwemo mkongwe Mike Barasa katika safu ya ushambuliaji.
Kocha msaidizi wa Simba, Amri Said 'Jaap Stam' ameiambia Alasiri jana kuwa vijana wake wapo katika hali nzuri kwa silimia 99 na kwamba kuifunga Yanga pekee haitoshi bali inataka kuvikwa taji.
"Pamoja na kwamba Simba inaongoza kwa kulitwaa kombe hilo, lakini kitendo cha kukutana na Yanga katika hatua yoyote ni changamoto ya kipekee inayoisukuma Simba kushinda," alisema.
Alisema kuifunga Yanga katika mchezo wa leo kuna maana kubwa mbili, kwanza kutaiwezesha Simba kutinga fainali na pili kutaifanya imalize mwaka vizuri.
Amri alisema katika soka la Tanzania na nchi nyingine zenye mvuto wa mchezo huo, timu pinzani zinapokutana ni lazima ratiba za wapenzi zinavurugika kila mmoja akitaka kuiona.
"Sisi tunatambua hilo na ndiyo maana tumejiwekea malengo ya kushinda na baadaye kulitwaa kombe lenyewe," alisema.

1 comment:

  1. Dada Jacqueline
    Kwa niaba ya familia yangu na wapenda mema wote nakutakia kila lililo jema wakati huu wa sikukuu na usalama kuelekea mwaka mpya
    Baraka kwako

    ReplyDelete