Monday, December 28, 2009

SOFAPAKA yawanyatia wawili wa Mtibwa


KLABU ya soka ya SOFAPAKA kutoka Kenya, imewazimia wachezaji wawili wa timu ya Mtibwa Sugar.
Fununu zilizoifikia blog hii ni kwamba uongozi wa klabu hiyo umeridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na mabeki hao wa Mtibwa.
Wachezaji hao ambao wanaweza kulamba bingo hilo iwapo yatafikiwa makubaliano kati ya uongozi wa Mtibwa na Sofapaka ni Idrisa Rajabu na Abdulhim Amour.
Habari zilizopatikana ni kwamba endapo uongozi huo utafanikiwa kuwasajili wachezaji hao itawatumia kwa ajili ya mashindano ya Klabu Bingwa Afrika.

No comments:

Post a Comment