Tuesday, December 1, 2009

Wasomi kuchuana Tanga

Na Renatha Msungu
SHIRIKISHO la michezo ya vyuo vikuu Tanzania (TUSA) limeandaa mashindano ya michezo ya Vyuo Vikuu yaliyopangwa kufanyika kesho hadi Desemba 11 katika viwanja vya Mkwakwani vilivyopo jijini Tanga.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Syllersaid Mziray alisema mechi ya ufunguzi katika mashindano hayo ambayo mgeni rasmi atakuwa mkuu wa mkoa wa Tanga Said Kalembo itakuwa kati ya timu ya UDSM, na ST Stephano.
Mziray ameitaja michezo itayochezwa kwenye mashindano hayo kuwa ni soka, netiboli, mpira wa kikapu, Wavu, Meza, Riadha na mchezo wa kuvuta kamba.Amesema jumla ya wanafunzi 700 wanatarajia kushiriki katika mashindano hayo ambayo yatashirikisha timu za wanawake na wanaume kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.
Mziray amesema mabingwa watetezi kwa upande wa soka ni ni timu ya UDSM, wakati kwa upande mpira wa Wavu ni Chuo cha Ardhi, huku mpira wa Kikapu ni timu ya TUDARCO, na netiboli ni chuo cha Makumira na kwa upande wa Riadha ni UDSM.
Amevitaja vyuo ambavyo vimethibitisha kushiriki katika mashindano hayo kuwa ni Chuo cha Ardhi, Chuo Kikuu Huria, UDSM, SUZA, Chuo cha Zanzibar, Chuo Kikuu cha Tumaini cha Dar es Salaam, Tumaini Iringa, MUCOPS na DUCE.
Vyuo vingine Chuo cha Mount Meru, Makumira, MUCE, KCMC, Kairuki, Mzumbe, SUA, UDOM na ST John.Wakati huo huo, TUSA imevitaka vyuo ambavyo bado havijathibitisha ushiriki wao kuthibitisha kabla ya tarehe ya kuanza kwa mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment